728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, November 28, 2015

    KILI STARS YABANWA NA ETHIOPIA,ROBO FAINALI YAWAKUTANISHA TENA

    Addis Ababa,Ethiopia.

    Kilimanjaro Stars imemaliza michezo ya hatua ya makundi ya Cecafa baada ya jioni ya leo kutoka sare ya goli 1-1 na wenyeji Ethiopia katika mchezo wa kundi A uliopigwa katika dimba la Awassa.

    Kilimanjaro Stars ilipata goli dakika ya 58 kupitia kwa Simon Msuva kabla ya Ethiopia kusawazisha dakika ya 92 kwa goli la kujifunga la mlinzi Salim Mbonde.

    Katika mchezo mwingine Uganda imefuzu boro fainali baada ya kuifunga Burundi kwa bao 1-0 lililofungwa na Frank Kalanda dakika ya 70.

    Wakati huohuo ratiba ya michuano ya robo finali imetolewa jioni ya leo ambapo Kilimanjaro Stars itavaana tena na Ethiopia.Ratiba iko kama ifuatavyo....

    Jumatatu

    Uganda v Malawi
    Tanzania v Ethiopia

    Jumanne

    South Sudan v Sudan
    Rwanda v Kenya

     

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KILI STARS YABANWA NA ETHIOPIA,ROBO FAINALI YAWAKUTANISHA TENA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top