728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, November 25, 2015

    LIGI YA MABINGWA ULAYA:ARSENAL,CHELSEA MAMBO SAFI,BAYERN,BARCA ZAFANYA MAUAJI


    London,England.

    Arsenal imefufua matumaini ya kutinga hatua ya 16 bora ya michuano ya vilabu bingwa barani Ulaya baada ya usiku wa leo kuilaza Dynamo Zagreb kwa jumla ya mabao 3-0.

    Arsenal ikiwa katika dimba lake la nyumbani la Emirates imepata magoli yake kupitia kwa Mesut Ozil na Alexis Sanchez aliyefunga mara mbili.

    Kufuatia ushindi huo Arsenal inakuwa imefikisha pointi sita ikihitaji kuifunga Olympiacos ambayo leo imekutana na kichapo cha mbwa mwizi baada ya kubamizwa magoli 4-0 na Bayern Munich katika mchezo uliopigwa katika dimba la Allianz Arena.

    Magoli ya Bayern Munich yamefungwa na Douglas Costa,Robert Lewandowski,Thomas Muller na Kingsley Coman huku mlinzi Holger BudStuber akilimwa kadi nyekundu kwa mchezo mbaya.

    Katika mchezo mwingine Chelsea imeifunga Maccabi Tel Aviv kwa jumla ya magoli 4-0 wafungaji wakiwa ni Garry Cahill,Willian,Oscar na Kurt Zouma.

    Kwingineko Barcelona imeinyuka AS Roma kwa jumla ya magoli 6-1.Magoli ya Barcelona yamefungwa na Louis Suarez aliyefunga mawili,Lionel Messi,Adriano Correa na Gerrard Pique huku Edin Dzeko akiifungia AS Roma goli la kufutia machozi.

    Matokeo mengine 

    Zenit St 2-0 Valencia
    BATE 1-1 Bayer Leverkusen
    Porto 0-2 Dynamo Kiev
    Lyon 1-2 Genk



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: LIGI YA MABINGWA ULAYA:ARSENAL,CHELSEA MAMBO SAFI,BAYERN,BARCA ZAFANYA MAUAJI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top