728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, January 03, 2015

    PODOLSKI ATUA INTER AAHIDI KUIREJESHA LIGI YA MABINGWA

    Milan,Italia.

    Ikiwa ni siku mbili tu tangu kufunguliwa kwa
    dirisha la usajili barani ulaya timu ya soka ya
    Inter milan imeonekana kuanza mwaka vyema
    kwa kuweka sawa safu ya ushambuliaji kwa
    kumsajili mshambuluaji wa Arsenal Lukas
    Podolski.

    Mjerumani huyo mshindi wa kombe la dunia mwenye umri wa miaka 29
    anakua mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Inter Milan iliyo chini ya Kocha Roberto Mancini.

    Podolski  alitua Milan jana ijumaa na leo jumamosi atafanyiwa vipimo vya afya kabla ya kuivaa Juventus siku ya jumanne katika mchezo wa ligi ya Seria A.

    Podolski anatumia Inter kwa  mkataba wa mkopo wa miezi sita ambao utaiingizia Arsenal kitita cha €600,000 kama ada ya uhamisho  ambayo inaweza kupanda na kufikia €850,000 ikiwa Inter itafuzu michuano ya Europa na ikiwa Inter itafuzu ligi ya mabingwa
    Arsenal itavuna €1milioni.

    Baada ya kutua Inter Podolski amesema

    ``Nimeongea na kocha Manchini.Nadhani ni kocha mzuri.

    Simfahamu vizuri lakini naifahamu vyema ligi ya Seria A.Nataka kuisaidia timu ifuzu ligi ya mabingwa"

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PODOLSKI ATUA INTER AAHIDI KUIREJESHA LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top