728x90 AdSpace

Wednesday, January 21, 2015

COPA DEL REY:LEO NI BARCA vs ATL MADRID

Uchambuzi na King
MUDA: Saa 6 usiku.
Leo katika dimba la Nou Camp jijini Barcelona kutakuwa bonge moja la mechi ya wababe wa La Liga Barca vs A.Madrid.
Msimu uliopita , Diego Simeone aliiongoza Atletico Madrid kumaliza ngebe za Barca
na Real za kutwaa Ubingwa wa Spain kwa Miaka 10 baada ya kutoka Sare 1-1 na Barca Uwanjani Nou Camp katika Mechi ya mwisho ya La Liga na wao kutwaa Ubingwa .
Kwenye Raundi iliyopita ya Copa del Rey Wiki iliyopita , Atletico Madrid waliwabwaga
Mahasimu wao wakubwa Real Madrid,ambao ndio walikuwa Mabingwa Watetezi , kwa Jumla ya Bao 4-2 katika Mechi mbili.
Atletico waliishinda Real Mechi ya kwanza 2-0 Nyumbani kwao Vicente Calderon na kutoka Sare 2-2 huko Santiago Bernabeu.
Hata hivyo , Barcelona iliifumua Elche kwa jumla ya bao 9-0 kwenye Copa del rey  na  kuwabamiza Atletico  Bao 3- 1
huko Nou Camp kwenye Mechi
ya La Liga Mapema Mwezi huu .
Licha ya kipigo hicho , Diego Simeone, Raia wa Argentina , ametamba kuibamiza Barca  kwenye mchezo wa leo .
Kwa ujumla huu ni mchezo ambao kila timu itakuwa ikihitaji kushinda ili kujiweka vizur kabla ya mechi ya marudiano hapo baadae.
...Subir dk90 uone vitu vitamu..
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: COPA DEL REY:LEO NI BARCA vs ATL MADRID Rating: 5 Reviewed By: Unknown