728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, January 18, 2015

    AMAVUBI KUTUA NCHINI JANUARI 21

    Timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi) itawasili Mwanza, Tanzania Januari 21 mwaka huu kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Taifa Stars Maboresho itakayochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini humo.

    Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Boniface
    Wambura, Amavubi yenye msafara wa watu 26, wakiwemo wachezaji, benchi la ufundi na
    viongozi itawasili kwa ndege ya RwandAir na siku hiyo hiyo jioni itafanya mazoezi kwenye
    Uwanja wa CCM Kirumba.

    Timu hiyo itafikia kwenye hoteli ya JB Belmont.Baada ya kocha Mdachi, Mart Nooij kutaja kikosi, Stars inaingia kambini keshokutwa (Januari 18 mwaka huu), na siku inayofuata
    itakwenda Mwanza tayari kwa ajili ya mechi hiyo itakayofanyika Januari 22 mwaka huu.

    Kikosi hicho cha Kocha Mart Nooij ambacho ni sehemu ya maandalizi ya mechi za mchujo
    za michuano ya Afrika kwa Wachezaji wanaocheza Ligi za Ndani (CHAN) kinaundwa
    na wachezaji 26.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: AMAVUBI KUTUA NCHINI JANUARI 21 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top