728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, January 21, 2015

    MPYA ZA USAJILI JUMATANO YA LEO TAR 21

    Tiote:Habari zinasema klabu ya Arsenal imefanya mazungumzo na wakala wa kiungo wa Newcastle Cheick Tiote 28 kwa ajili ya kumsajili januari hii.Tiote inataka mshahara wa £80,000 na mkataba wa miaka mitatu na nusu.

    Quadrado:Klabu ya Chelsea imeripotiwa kuanza mazungumzo ya kumnasa nyota wa klabu ya Fiorentina raia wa Colombia Juan Quadrado mwenye thamani ya £28m.

    Drimic:Klabu ya Bayern Leverkusen imeripotiwa kutaka mshambuliaji wa klabu ya Tottenham Roberto Soldado na katika kuharakisha usajili huo iko tayari kutoa pesa na mshambuliaji wake Mswisi Josep Drimic.

    Kane:Klabu ya Tottenham inajipanga kumpunguzia mzigo wa kufunga magoli nyota wake Harry Kane kwa kusajili washambuliaji wengine wapya.Wanaotajwa sana ni Jay Rodriquez na Carlos Bacca.

    Cavani:Mshambuliaji wa klabu ya Psg Edinson Cavani ameonyesha kupendelea zaidi kuhamia klabu ya Arsenal kuliko vilabu vya Manchester United na Liverpool hapo majira ya joto.

    Paulista:Taarifa kutoka vyombo vingi vya habari nidai kuwa klabu ya Arsenal iko katika hatua nzuri ya kumnasa mlinzi wa Villarreal Gabriel Paulista 24 baada ya kukubali kutoa ada ya £10m.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MPYA ZA USAJILI JUMATANO YA LEO TAR 21 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top