728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, January 14, 2015

    ANGELO ATIMKA UNITED,FLETCHER KUFUATIA

    Angelo Henriquez:Kocha mkuu wa klabu ya Dinamo Zagreb  ya Croatia Zoran Mamic ametangaza kuwa klabu yake imekamilisha usajili wa mshambuliaji kinda wa klabu ya Manchester United raia wa Chile Angelo Henriquez (19) kwa mamilioni ya Euro.
    Henriques ambaye kabla ya uhamisho huo wa kudumu alikuwa akiichezea Zagreb kwa mkopo na kufanikiwa kuifungia jumla ya magoli 15 katika michezo 18 ya ligi ya Croatia msimu huu.
    Manchester United ilimsajili Angelo mwaka 2012 toka klabu ya Universidad de Chile kwa ada ya£4m.


    Darren Fletcher:Klabu ya Westbrom Wich Albion
    imeulizia uwezekano wa kumsajili kiungo mkongwe wa klabu ya Manchester United Darren Fletcher (30).
    West brom inataka kumsajili kiungo huyo ili kwenda kuongeza nguvu baada ya kiungo wake Youssuf Mulumbu kuwa katika majukumu ya kuitumikia timu yake ya Drc Congo katika michuano ya AFCON inayotarajiwa kuanza hivi karibuni huko Equatorial Guinea.
    Fletcher ni kati ya nyota wa Manchester United wanaohaha kupata nafasi ya kucheza kikosi cha kwanza kwani katika msimu huu amebahatika kuanza jumla ya michezo mitatu tu chini ya kocha Louis Van Gaal.
    Fletcher amekuwa Manchester United kwa miaka 12 sasa huku akifanikiwa kutwaa jumla ya mataji matano ya ligi kuu na moja la ligi ya mabingwa  Ulaya.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ANGELO ATIMKA UNITED,FLETCHER KUFUATIA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top