728x90 AdSpace

Monday, January 19, 2015

AFCON:MDUDU SARE ATAWALA,LEO NI SENEGAL v GHANA.

Ebebiyin.

Michuano ya AFCON iliendelea tena jana jumapili kwa michezo miwili ya kundi B iliyopigwa katika dimba la Nuevo Estadio de Ebebiyín.

Katika mchezo wa mchezo wa mapema Zambia na Congo DRC ziligawana pointi baada ya kutoka sare ya goli 1-1.Goli la Zambia lilifungwa na Given Singuluma kabla ya Yennick kuisawazishia Congo.

Katika mchezo wa pili sare pia iliendelea kutawala baada ya Tunisia na Cape Verde kufungana goli 1-1.Goli la Tunisia lilifungwa na Mohamed Manser huku Cape Verde wakisawazisha kwa mkwaju wa penati ulifungwa na Almeida Heldon.

Leo jumatatu kutakuwa na mechi mbili za kundi C ambapo Ghana watacheza na Senegal huku Algeria wakivaana baadae na Afrika ya Kusini.

Mechi ambazo zote zitapigwa katika dimba la Estadio de Mongomo,Mjini Mongomo .
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: AFCON:MDUDU SARE ATAWALA,LEO NI SENEGAL v GHANA. Rating: 5 Reviewed By: Unknown