728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, January 19, 2015

    AFCON:MDUDU SARE ATAWALA,LEO NI SENEGAL v GHANA.

    Ebebiyin.

    Michuano ya AFCON iliendelea tena jana jumapili kwa michezo miwili ya kundi B iliyopigwa katika dimba la Nuevo Estadio de Ebebiyín.

    Katika mchezo wa mchezo wa mapema Zambia na Congo DRC ziligawana pointi baada ya kutoka sare ya goli 1-1.Goli la Zambia lilifungwa na Given Singuluma kabla ya Yennick kuisawazishia Congo.

    Katika mchezo wa pili sare pia iliendelea kutawala baada ya Tunisia na Cape Verde kufungana goli 1-1.Goli la Tunisia lilifungwa na Mohamed Manser huku Cape Verde wakisawazisha kwa mkwaju wa penati ulifungwa na Almeida Heldon.

    Leo jumatatu kutakuwa na mechi mbili za kundi C ambapo Ghana watacheza na Senegal huku Algeria wakivaana baadae na Afrika ya Kusini.

    Mechi ambazo zote zitapigwa katika dimba la Estadio de Mongomo,Mjini Mongomo .
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: AFCON:MDUDU SARE ATAWALA,LEO NI SENEGAL v GHANA. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top