728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, January 13, 2015

    KOCHA JULIO ADUNDWA MUSOMA

    Musoma,Tanzania.

    Kocha wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amekumbana na balaa mjini Musoma.

    Julio amepigwa jiwe na kujeruhiwa wakati timu yake ya Mwadui FC ikicheza mechi ya Ligi Daraja la Kwanza dhidi ya Polisi Mara.

    Mechi hiyo ilichezwa wikiendi mjini Musoma na kumalizika kwa sare ya mabao 2-2.

    Hali hiyo ilisababisha mashabiki wa Polisi kuanza kuwashambulia Julio na wachezaji wake ambao baadhi walijeruhiwa.

    “Kweli nimepigwa jiwe la mgongoni na sasa siko vizuri. Nimeshindwa hata kwenda mazoezini.

    “Hakika hawakututendea haki na
    askari polisi hawakuwa na msaada,” alisema Julio.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KOCHA JULIO ADUNDWA MUSOMA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top