728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, January 19, 2015

    TAARIFA ZOTE MPYA ZA USAJILI ZIKO HAPA

    Icardi akiwajibika dimbani
    Dirk Kuyt:Vilabu vya Ac Milan,Westham United,Lyon na Valencia vimeripotiwa kuisaka saini ya mshambuliaji wa klabu ya Fenerbahce ya Uturuki Dirk Kuyt 34 anayemaliza mkataba mwezi juni.

    Mauro Icardi:Vilabu vya Liverpool na
    Chelsea kwa pamoja vimeripotiwa kuanza kumfukuzia mshambuliaji kinda wa Inter Milan Mauro Icardi 21 mwenye thamani ya £26m.Icardi ameifungia Inter magoli 10 katika michezo 18.

    Lukas:Kiungo wa klabu ya Liverpool Mbrazil Lukas Leiva ameripotiwa kuichoka klabu hiyo na anafanya kila awezalo atimke januari hii na kutua Inter Milan ya Italia.

    Bishop:Klabu ya Liverpool imeripotiwa kuwa mbele kabisa katika mbio za kumnasa kiungo kinda wa klabu ya Ipswich town Teddy Bishop 18.

    Xavi:Kiungo wa klabu ya Barcelona ya Hispania Xavi Hernandez amewataka viungo wenzie wa Kispania Santi Cazorla na David Silva kuja kucheza katika klabu hivyo kwa kuwa wana sifa zote zinazotakiwa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TAARIFA ZOTE MPYA ZA USAJILI ZIKO HAPA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top