728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, May 11, 2017

    Arsenal yaifumua Southampton na kuirejesha Man United nafasi ya sita


    Southampton,England.

    ARSENAL imefanikiwa kuirejesha Manchester United mpaka nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi kuu ya soka nchini England baada ya usiku huu ikiwa ugenini St.Mary's kuwafunga wenyeji wao Southampton kwa mabao 2-0 kwenye mchezo wa kiporo.

    Katika mchezo huo uliochezeshwa na mwamuzi John Moss ilishuhudiwa Arsenal ikijipatia mabao yake yote kipindi cha pili kupitia kwa Alexis Sanchez aliyefunga bao la kwanza katika dakika ya 60 kabla ya Olivier Giroud kuongeza la pili kwa kichwa katika dakika ya 84.


    Ushindi huo umeifanya Arsenal ichupe mpaka nafasi ya tano baada ya kufikisha pointi 66.Pointi moja zaidi ya Manchester United ambayo sasa imeshuka mpaka nafasi ya sita ikiwa na pointi zake 65.




    Aidha katika mchezo huo Arsenal ilipata pigo baada ya kulazimika kufanya mabadiliko ya lazima kufuatia winga wake Alex Oxlade Chamberlain kupata jeraha la misuli ambalo linahofiwa kuenda likamweka nje ya dimba mpaka mwisho wa msimu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Arsenal yaifumua Southampton na kuirejesha Man United nafasi ya sita Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top