728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, June 05, 2016

    KUSAKA TIKETI YA AFCON:KENYA YAICHAPA CONGO BRAZZAVILLE 2-1 NYUMBANI NA KUIPELEKA GUINEA BISSAU GABON.



    NAIROBI, Kenya.


    MABAO mawili ya kila kipindi ya washambuliaji Ayub Timbe na Eric Johanna yameipa Harambee Stars ushindi  mabao 2-1 nyumbani dhidi ya wageni Congo Brazzaville katika mchezo mkali wa kusaka tiketi ya kushiriki michuano ya AFCON hapo mwakani nchini Gabon.

    Katika mchezo huo ulioisha hivi punde katika uwanja wa Safaricom/Moi Kasarani wageni Congo Brazzaville ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza dakika ya 19 baada ya nahodha wake Oniangue kufunga kwa mkwaju wa penati uliopatikana baada ya Ferebory Dore kuangushwa ndani ya boksi na kiungo wa Kenya Ismail Gonzalez.
     Harambee Stars players cerebrating after scoring the second goal.PHOTO/Raymond Makyaha.
    Baada ya kuingia kwa bao hilo Kenya iliamka na kuanza kulisakama lango la Congo Brazzaville na ilipofika dakika ya 27 juhudi zao zilizaa matunda baada ya Ayub Timbe kufunga bao la kusawazisha baada ya kuwazidi mbio walinzi wa Congo Brazzaville.Bao la ushindi limefungwa Eric Johanna dakika ya 61.
     Harambee Stars midfielder Francis Kahata attempting to block a shot from a Congo player.PHOTO/Raymond Makhaya.
    Kwa matokeo hayo Guinea Bissau ambayo iliifunga Kenya nyumbani na ugenini imefuzu fainali zake za kwanza za AFCON baada ya Jana Jumamosi kuifunga Zambia kwa mabo 3-2  huko Bissau na kufikisha pointi 10 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote ile katika kundi hilo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KUSAKA TIKETI YA AFCON:KENYA YAICHAPA CONGO BRAZZAVILLE 2-1 NYUMBANI NA KUIPELEKA GUINEA BISSAU GABON. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top