728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, June 11, 2016

    EURO 2016:WENYEJI UFARANSA WAANZA KWA USHINDI,ENGLAND,WALES DIMBANI LEO RATIBA/MUDA YOTE VIKO HAPA

    Paris,Ufaransa.

    UFARANSA imeianza vyema michuano ya Euro 2016 baada ya Ijumaa usiku kuifunga Romania kwa mabao 2-1 katika mchezo mkali wa ufunguzi wa Kundi A uliochezwa katika uwanja wa Stade de France,Paris.

    Ufaransa ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza dakika ya 57 ya kipindi cha pili baada ya Olivier Giroud kufunga kwa kichwa safi.Giroud alifunga bao hilo akimalizia krosi ya Dimitri Payet iliyomshinda kipa wa Romania Ciprian Tatarusanu.


    Dakika ya 65 Bogdan Stancu aliifungia Romania bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penati.Penati hiyo ilitolewa na mwamuzi Victor Kassai baada ya Nicolae Stanciu kuangushwa ndani ya boksi na mlinzi wa kushoto wa Ufaransa Patrice Evra.

    Mchezo ukiwa unaelekea ukingoni,dakika ya 89 Dimitri Payet aliifungia Ufaransa bao la ushindi kwa mkwaju mkali wa mguu wa kushoto na kufanya Ufaransa imetoke kifua mbele kwa mabao 2-1.

    VIKOSI

    Starting XI
    France XI: Lloris; Sagna, Rami, Koscileny,
    Evra; Matuidi, Pogba, Kanté; Payet,Giroud, Greizmann

    Romania XI: Tătăruşanu, Săpunaru,Grigore, Chiricheş, Raţ, Hoban, Pintilii,Stanciu, Popa, Stancu, Andone

    Ratiba ya leo Jumamosi Juni 11,2016.

    Kundi A
    Albania v Uswisi (16:00)

    Kundi B
    Wales v Slovakia (19:00)
    England v Urusi (22:00)hh
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: EURO 2016:WENYEJI UFARANSA WAANZA KWA USHINDI,ENGLAND,WALES DIMBANI LEO RATIBA/MUDA YOTE VIKO HAPA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top