728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, June 11, 2016

    EURO 2016:USWISI YAWACHAPA MAJIRANI ZAO ALBANIA

    Paris,Ufaransa.

    USWISI imeianza vyema michuano ya Euro 2016 baada ya jioni ya leo kuwachapa majirani zao Albania kwa bao 1-0 katika mchezo mkali wa Kundi A uliochezwa katika uwanja wa Stade Bollaert-Delelis.

    Bao pekee la mchezo huo
    limefungwa dakika ya tano kwa kichwa na mlinzi Fabian Schar.Schar alifunga bao hilo akitumia makosa ya kipa wa Albania Etrit Berisha aliyeshindwa kuuwahi mpira wa kona uliopigwa na Xherdan Shaqiri.

    Dakika ya 37 Albania ilipata pigo baada ya nahodha wake Lorik Cana kulimwa kadi nyekundu baada ya kushika mpira kwa maksudi.

    Kwa matokeo hayo Uswisi imefikisha pointi tatu ikiwa sawa na wenyeji Ufaransa ambao jana Ijumaa waliifunga Romania kwa mabao 2-1 huko Stade de France.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: EURO 2016:USWISI YAWACHAPA MAJIRANI ZAO ALBANIA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top