728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, June 04, 2016

    COPA AMERICA:WENYEJI MAREKANI WAANZA VIBAYA,WACHAPWA 2-0 NA COLOMBIA

    Santa Clara,Marekani.

    Wenyeji timu ya taifa ya Marekani wameianza vibaya michuano ya Copa America Centenario baada ya alfajiri ya leo kukubali kichapo cha mabao 2-0 toka kwa timu ya taifa ya Colombia katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi A uliochezwa katika uwanja wa Levi's Stadium,Santa Clara.

    Mabao yaliyoipa ushindi huo muhimu Colombia yamefungwa dakika za 8 na 42 kupitia kwa mlinzi wake Christian Zapata na mshambuliaji wake James Rodriguez..

    Rodriguez alifunga bao hilo kwa mkwaju wa penati uliotolewa na mwamuzi Roberto Garcia baada ya mlinzi wa Marekani DeAndre Yedlin kushika mpira ndani ya boksi.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: COPA AMERICA:WENYEJI MAREKANI WAANZA VIBAYA,WACHAPWA 2-0 NA COLOMBIA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top