728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, June 13, 2016

    BUFFON AKISTAAFU NA MIMI NITASTAAFU

    Paris,Ufaransa. 

    KIPA na nahodha wa Hispania Iker Casillas amesema hatastaafu mchezo wa soka mpaka pale kipa na nahodha wa timu ya taifa ya Italia, Gianluigi Buffon atakaposema imetosha yaani amestaafu.

    Akiongea na jarida la michezo la Italia la La Gazzetta dello Sport,kutokea nchini Ufaransa  alikokwenda kuitumikia Hispania katika michuano ya Ulaya (Euro) Casillas,35, amesema haoni sababu ya kustaafu kwasasa wakati wachezaji wenye umri mkubwa kuliko yeye kama swahiba wake,Gianluigi Buffon bado wanatamba viwanjani.

    Amesema "Kuhusu kustaafu!!Nadhani Buffon atakapostaafu,nitastaafu pia. 

    "Amesaini mkataba mpya hivi karibuni na hilo litanifanya niwe na furaha
    kwa sababu nina imani na mimi nitasaini pia.

    "Muda wetu wa kustaafu utakapofika,tutaandaa mchezo kati ya marafiki zangu na marafiki zake kuhitimisha zama zetu"

    Kauli hiyo ya Casillas imekuja baada ya hivi karibuni Buffon,38, kusaini mkataba mpya wa miaka miwili katika klabu yake ya Juventus.Mkataba huyo mpya utamfanya Buffon aendelee kucheza soka la ushindani mpaka atakapofikisha umri wa miaka 40 hapo mwaka 2018.

    Kwasasa Casillas anaichezea FC Porto ya Ureno na ana kipengele katika mkataba wake kinachomruhusu kuendelea kucheza mpaka mwaka 2018.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BUFFON AKISTAAFU NA MIMI NITASTAAFU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top