728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, May 14, 2017

    Mputu atupia,TP Mazembe ikianza vyema makundi shirikisho

    Lubumbashi,Congo.

    TP Mazembe imeanza vyema kuutetea ubingwa wake wa kombe la shirikisho Afrika baada ya jioni ya leo kuitambia CF Mounana ya Gabon kwa kuifunga mabao 2-0 kwenyemchezo wa kwanza wa kundi D uliochezwa kwenye uwanja wa Stade TP Mazembe huko Lubumbashi. 

    Ushindi huo umeipeleka TP Mazembe kileleni mwa msimamo wa kundi D baada ya kufikisha pointi tatu kufuatia kushuka dimbani mara moja. CF Mounana inashika mkia kwenye kundi hilo.

    Ilimchukua dakika 18   Tresor Mputu Mabi kuifungia TP Mazembe bao la kuongoza akitumia vyema pasi ya. Issama  Mpeko.Bao hilo lilidumu mpaka mapumziko. Kipindi cha pili nahodha Rainford Kalaba aliipa TP Mazembe uhakika wa kuibuka na pointi tatu baada ya kufunga bao la pili baada ya kazi nzuri ya Mazembe Solomon Asante
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Mputu atupia,TP Mazembe ikianza vyema makundi shirikisho Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top