728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, June 12, 2016

    EURO 2016:ENGLAND YAUSHINDWA MZIKI WA URUSI YALAZIMISHWA SARE YA 1-1 MARSEILLE,ROONEY MCHEZAJI BORA

    Marseille,Ufaransa.

    BAO la dakika ya 92 la nahodha Vasili Belezutski limeinyima England ushindi baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Urusi katika mchezo mkali wa Kundi B wa michuano ya Euro 2016 uliochezwa Jumamosi usiku katika uwanja wa Stade Veledrome ulioko Marseille.


    England ndiyo walikuwa wa kwanza kufunga dakika ya 73 kupitia kwa kiungo wake Eric Dier,lakini nahodha Vasili Belezutski akaisawazishia Urusi dakika ya 92 na kufanya mchezo uishe kwa sare ya bao 1-1.

    England itarejea tena dimbani Alhamis kuvaana na ndugu zao Wales huku Urusi wakicheza na Slovakia siku ya Jumatano.

    VIKOSI

    England: Hart, Walker, Cahill, Smalling, Rose,Alli, Dier, Rooney, Sterling, Kane, Lallana.

    Akiba: Wilshere, Milner.


    Russia: Akinfeev, Smolnikov, V.Berezutski,Ignashevich, Schennikov, Neustadter, Golovin,Kokorin, Shatov, Smolov, Dzyuba.

    Akiba: Glushakov, Mamaev, Shirokov.

    Mchezaji Bora wa mechi: Wayne Rooney

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: EURO 2016:ENGLAND YAUSHINDWA MZIKI WA URUSI YALAZIMISHWA SARE YA 1-1 MARSEILLE,ROONEY MCHEZAJI BORA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top