728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, June 06, 2016

    COPA AMERICA CENTENARIO KUNDI C:URUGUAY YALIMWA 3-1 NA MEXICO,KADI NYEKUNDU TATU ZATOKA,JAMAICA CHALI

    Arizona,Marekani.

    TIMU ya taifa ya Uruguay ikiwa bila ya nyota wake Luis Suarez imeianza vibaya michuano ya kumsaka bingwa wa kombe la Copa America Centenario baada ya alfajiri ya leo kufungwa mabao 3-1 na timu ya taifa ya Mexico katika mchezo mkali wa kundi C uliochezwa katika uwanja wa University
    of Phoenix Stadium huko Arizona,Marekani.

    Jahazi la Uruguay lilianza kwenda kombo dakika ya 4 tu ya mchezo baada ya mlinzi wake Alvaro Perreira kujifunga akiwa katika harakati za kuokoa hatari langoni mwake.

    Dakika ya 74 nahodha Diego Godin aliisawazishia bao Uruguay ambalo halikuwa na msaada sana kwani Mexico walikuja juu na kufunga mabao mawili ya haraka haraka kupitia kwa Rafa Marquez dakika ya 85 na Hector Herrera dakika ya 90 na kufanya mchezo uishe kwa Mexico kushinda kwa mabao 3-1dhidi ya Uruguay.

    KADI NYEKUNDU

    Mexico na Uruguay zililazimika kumaliza mchezo zikiwa na wachezaji pungufu baada ya wachezaji wao kulimwa kadi nyekundu kwa michezo mibaya.Matias Vecino 45' kwa Uruguay na Andres Guardado 73' kwa Mexico.

    VIKOSI

    México: Talavera; Araujo, Reyes, Moreno,
    Layún; Herrera, Márquez, Guardado;Aquino, Hernández, Corona.

    Uruguay: Muslera; M.Pereira, Godín,
    Giménez, A.Pereira; C.Sánchez, A.Ríos,
    Vecino, Rolan; Lodeiro, Cavani.

    Katika mchezo wa mapema wa Kundi C uliochezwa katika uwanja wa jeshi, Chicago, Illinois ,Venezuela ilichomoza na ushindi baada ya kuilaza Jamaica kwa bao 1-0 lililofungwa dakika ya 15 na Josef Martinez baada ya kupokea pasi maridadi toka kwa Alejandro Guerra. Dakika ya Jamaica ilipata pigo baada ya mlinzi wake Rudolf Austin kulimwa kadi nyekundu kwa mchezo mbaya.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: COPA AMERICA CENTENARIO KUNDI C:URUGUAY YALIMWA 3-1 NA MEXICO,KADI NYEKUNDU TATU ZATOKA,JAMAICA CHALI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top