728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, June 13, 2016

    BRAZIL OUT COPA AMERICA CENTENARIO,REKODI YA 1987 YAJIRUDIA TENA

    Massachusetts,Marekani.

    BRAZIL imetupwa nje ya michuano ya Copa America Centenario baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0 toka kwa Peru katika mchezo mkali wa Kundi B uliochezwa katika uwanja wa Gillette Stadium, Foxborough,Massachusetts.

    Bao pekee la mchezo huo limefungwa dakika ya 75 na Raul Ruidiaz.Rudiaz aliyekuwa ameingia akitokea benchi alifunga bao hilo kwa mkono akiunganisha pasi ya Andy Polo. 

    Kuingia na kukubaliwa kwa bao hilo kulimweka matatani mwamuzi Andres Cunha toka Uruguay baada ya wachezaji wa Brazil kumzonga na kumtaka afute bao hilo kwa madai mfungaji alitumia mkono kufunga.

    Hii ni mara ya kwanza kwa Brazil kuondolewa katika hatua ya makundi ya michuano ya Copa America mara ya mwisho ilikuwa ni mwaka1987.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BRAZIL OUT COPA AMERICA CENTENARIO,REKODI YA 1987 YAJIRUDIA TENA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top