728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, January 05, 2015

    KOMBE LA MAPINDUZI:YANGA,AZAM ZATOA VIPIGO

    Vilabu vya Yanga na Azam vimeendelea kukusanya pointi baada ya vyote viwili kushinda michezo yake ya kombe la Mapinduzi.

    Katika mchezo wa mapema Yanga iliibuka na ushindi mnene dhidi ya Polisi Zanzibar baada ya kuwafunga maafande hao kwa jumla ya magoli 4-0.

    Magoli ya Yanga yalifunga na Mbrazil Andre Coutinho aliyefunga mara mbli,mshambuliaji Akpah Sherman na winga Simon Msuva.

    Katika mchezo wa mwisho Azam ilijipatia ushindi wa goli 1-0 dhidi ya KMKM na kufikisha pointi nne baada ya mchezo wake wa kwanza kutoka sare ya 2-2 na klabu ya KCCA.

    Matokeo Mengine
    KCCA 3-0 Mtende Fc
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KOMBE LA MAPINDUZI:YANGA,AZAM ZATOA VIPIGO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top