728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, May 16, 2017

    Kumbe Yanga ndiyo chanzo cha mvutano Simba SC


    Dar Es Salaam,Tanzania.

    KASHESHE kubwa linaendelea ndani ya Simba chanzo kikiwa ni mkataba mpya waliosaini na kampuni ya SportPesa ya Kenya, lakini uchunguzi wa Mwanaspoti jana Jumatatu umebaini tatizo jipya.

    Simba ilisaini mkataba huo wa miaka mitano Ijumaa iliyopita ukiwa na thamani ya Sh4.96 bilioni ambapo kwa mwaka watakuwa wanachukua Sh888 milioni pamoja na bonasi mbalimbali ambazo zitatokana na ufanisi wao kwenye mashindano ya ndani na nje ya nchi.

    Mara baada ya kusainiwa mkataba huo, juzi Jumapili vigogo wa Simba akiwemo Zacharia Hanspoppe pamoja na mfadhili wa klabu hiyo, Mohammed Dewji ‘MO’ walitangaza kubwaga manyanga kwa maelezo kwamba hawakuhusishwa kwenye dili hilo.

    Lakini si hao tu, hata baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji nao wako kwenye hatihati ya kujiondoa kwa maelezo kwamba walionyeshwa baadhi ya vipengele vya mkataba huo siku moja kabla ya kusainiwa kwake, jambo ambalo wamedai ni kinyume na utaratibu wao wa kuendesha mambo.

    Pamoja na hayo yote, lakini uchunguzi wa Mwanaspoti ambayo ilikutana chemba na wajumbe kadhaa wa Simba juzi na jana ulibaini kuwa wamegundua kitu kwenye dili la Yanga na SportPesa.

    Habari zinasema kwamba wajumbe hao wamefanya uchunguzi wao na kubaini kuwa Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji amewakomalia SportPesa wakaipa Yanga dau kubwa kuliko wao. Habari zinasema kuwa Simba wamebaini Yanga itapewa dau la Sh950 milioni kwa mwaka tofauti na Mnyama ambaye Evans Aveva amesaini mkataba wa Sh888 milioni kwa mwaka.

    Hiyo inamaanisha kwamba Yanga watalamba zaidi ya Sh5 bilioni kwa miaka mitano.

    Ingawa SportPesa jana hawakuwa tayari kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu na hilo, lakini habari zinasema kwamba walipanga kusaini mkataba na Yanga leo Jumanne kwenye makao makuu pale Jangwani,  lakini wameahirisha kwasababu ambazo hatahivyo hazijawekwa wazi.

    Habari zinasema kwamba Simba wamebaini kwamba Manji alikuwa anagoma kutoa nembo yake ya Quality Group kifuani mwa jezi kwenda begani mpaka walipolazimika kuongeza fungu hilo ambalo Simba wanadai wamelishtukia.

    Wajumbe hao wa Simba wanadai kwamba MO alikuwa ameshafikia makubaliano na Acacia ambao walikuwa wasaini pale tu alipokuwa anaingia Simba kwa hisa asilimia 51. Wanadai kwamba Acacia walikuwa waipe Simba Sh2 bilioni kwa mwaka na nembo yao ikae kifuani ambapo sasa haiwezekani tena baada Aveva kusaini dili ya miaka mitano na SportPesa.

    VIKAO HAVIISHI

    Mwanaspoti linafahamu kwamba viongozi wa Simba kupitia Kamati ya Utendaji juzi Jumapili walikutana katika kikao cha dharura baada ya Hanspoppe kutangaza kujiuzulu na MO kutaka fedha zake alizoikopesha klabu hiyo ambazo ni Sh1.4 bilioni.

    Chanzo:Mwanaspoti
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Kumbe Yanga ndiyo chanzo cha mvutano Simba SC Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top