728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, May 19, 2017

    Ander Herrera mchezaji bora Man United,Valencia,Mkhitaryan,Gome,Tuanzebe wapeta

    Manchester,England.
    USIKU wa kuamkia leo kulikuwa na kazi moja tu jijini Manchester.Kazi hiyo haikuwa nyingine bali ni kuwatunuku mituzo kama si mizawadi wachezaji waliofanya kweli wakiwa na jezi ya Manchester United kwa msimu wa 2016/17.
    Kiungo Ander Herrera amehitimisha utawala wa miaka mitatu wa Mhispania mwenzake,David De Gea baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa msimu wa Manchester United.
    Herrera mwenye umri wa miaka 27 ametwaa tuzo hiyo kwa tofauti ya kura 242 dhidi ya mlinzi,Antonio Valencia aliyeshika nafasi ya pili.Nafasi ya tatu imeshikwa na Zlatan Ibrahimovic.
    Tokeo la picha la hererra wins player of the year awardAntonio Valencia ametwaa tuzo ya mchezaji bora chaguo la wachezaji huku Henrick Mkhitaryan akitwaa tuzo ya bao bora la msimu.Ni lile bao la maajabu la Scorpion Kick alilofunga mwezi Disemba dhidi ya Sunderland.Tokeo la picha la hererra wins player of the year award
    Axel Tuanzebe ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa kikosi cha akiba huku Angel Gomes ambaye ni mpya wa nyota wa zamani wa timu hiyo Luis Nani akitwaa tuzo ya mchezaji bora chipukizi.Tokeo la picha la hererra wins player of the year award
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Ander Herrera mchezaji bora Man United,Valencia,Mkhitaryan,Gome,Tuanzebe wapeta Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top