728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, August 05, 2016

    BRAZIL YAANZA KICHOVU OLYIMPIKI YALAZIMISHWA SARE NA AFRIKA KUSINI,MASHABIKI WAIZOMEA

    Brasilia,Brazil.

    BRAZIL imeanza kichovu harakati zake za kuisaka medali yake ya kwanza ya michuano ya Olyimpiki kwa upande wa soka la wanaume baada ya Alhamis Usiku kulazimisha sare ya bila kufungana na Afrika Kusini katika mchezo mkali wa kundi A uliochezwa katika Uwanja wa Mane Garrincha Stadium,Brasilia hali iliyofanya mashabiki wake kuizomea.


    Licha ya kuwa na safu kali ya ushambuliaji ikiongozwa na nahodha wake Neymar Jr,Gabriel Jesus na Gabriel Barbosa Gabigol ,Brazil imejikuta ikikosa mbinu za kuugusa wavu wa Afrika Kusini iliyolazimika kumaliza mchezo ikiwa pungufu baada ya mlinzi wake Mothobi Mvala kutolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 59 kwa mchezo mbaya.

    Matokeo Mengine 

    Kundi A

    Iraq 0-0 Denmark 

    Kundi B

    Colombia 2-2 Sweden

    Kundi C

    Mexico 2 -2 Ujerumani

    Kundi D

    Ureno 2-0 Argentina 

    Ratiba ijayo

    Jumapili

    Brazil v Iraq 
    Afrika Kusini v Denmark .

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BRAZIL YAANZA KICHOVU OLYIMPIKI YALAZIMISHWA SARE NA AFRIKA KUSINI,MASHABIKI WAIZOMEA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top