728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, August 30, 2016

    HAMIS KIIZA APATA TIMU AFRIKA KUSINI


    Hamis Kiiza

    Bethlehem,Afrika Kusini.

    MSHAMBULIAJI wa zamani wa vilabu vya Yanga SC na Simba SC,Mganda Hamisi Kiiza ‘Diego’ yupo katika hatua za mwisho kujiunga na klabu ya Free State Stars inayoshiriki ligi kuu ya nchini Afrika Kusini maarufu kama ABSA Premiership.

    Kiiza ambaye aliachwa na Simba SC msimu uliopita wa ligi kuu Tanzania bara kwa madai ya utovu wa nidhamu amefuzu majaribio ya wiki moja katika klabu hiyo na atasaini mkataba wa mwaka mmoja mara tu atakapopata hati ya uhamisho wa kimataifa (ITC) kutoka Shirikisho la soka Tanzania (TFF).

    Free State Stars ambayo ina makao yake makuu katika uwanja wa Goble Park inachezewa na Mtanzania,Mrisho Khalfani Ngasa.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: HAMIS KIIZA APATA TIMU AFRIKA KUSINI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top