728x90 AdSpace

Tuesday, August 23, 2016

CHELSEA,LIVERPOOL ZAFUZU HATUA YA 3 EFL


London, Uingereza.

MABAO mawili ya Mshambuliaji wa Ubelgiji, Michy Batshuayi,yameipa Chelsea ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Bristal Rovers katika mchezo mkali wa hatua ya nne ya michuano ya EFL (Kombe la Ligi) uliochezwa usiku huu katika uwanja wa Stamford Blidge.

Batshuayi alianza kuipa raha Chelsea baada ya kuifungia bao la kuongoza dakika ya 29 ya mchezo kabla ya dakika ya 31 Victor Moses kuongeza bao la pili.Bao la tatu la Chelsea limefungwa dakika ya 41 na Michy Batshuayi.




Mabao ya Bristal Rovers yamefungwa na Peter Hartley dakika ya 34 ya mchezo pamoja na Ellis Harrison aliyefunga bao la pili kwa mkwaju wa penati na kufanya mchezo uishe kwa Chelsea kutoka kifua mbele uwanjani kwa ushindi wa mabao 3-2.

Katika mchezo mwingine Liverpool ikiwa ugenini imechomoza na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Burton Albion shukrani kwa mabao ya Divock Origi,Roberto Firmino,Tom Naylor na Daniel Sturridge,aliyefunga mabao mawili.

Matokeo hayo yamezipeleka Chelsea na Liverpool hatua ya tatu ya michuano ya EFL

Matokeo Mengine ya EFL yako kama Ifuatavyo

Crystal Palace 2 - 0 Blackpool

Blackburn Rovers 3 - 3 Crewe Alexandra

Burton Albion 0 - 5 Liverpool

Chelsea 3 - 2 Bristol Rovers Derby County 1 - 1 Carlisle United

Everton 4 - 0 Yeovil Town

Exeter City 1 - 3 Hull City

Luton Town 0 - 1 Leeds United

Millwall 1 - 2 Nottingham Forest

Newcastle United 2 - 0 Cheltenham Town

Northampton Town 2 - 2 West Bromwich Albion

Norwich City 6 - 1 Coventry City
Oxford United 2 - 4 Brighton & Hove Albion

Peterborough United 1 - 3 Swansea City

Preston North End 2 - 0 Oldham Athletic

Queens Park Rangers 2 - 1 Rochdale

Scunthorpe United 1 - 1 Bristol City

Stevenage 0 - 4 Stoke City

Watford 1 - 1 Gillingham

Wolverhampton Wanderers Cambridge United

Reading 1 - 1 Milton Keynes.


  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: CHELSEA,LIVERPOOL ZAFUZU HATUA YA 3 EFL Rating: 5 Reviewed By: Unknown