728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, August 24, 2016

    LIGI KUU BARA:TOTO AFRICANS YAIZIMA MWADUI FC CCM KIRUMBA


    Mwanza,Tanzania.

    TOTO Africans imeuanza vyema msimu mpya wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) baada ya jioni ya leo kuishushia Mwadui FC kichapo cha bao 1-0 katika mchezo mkali uliochezwa katika uwanja wa CCM Kirumba,Mwanza.

    Bao la ushindi katika mchezo huo pekee wa ligi kuu Jumatano ya leo limefungwa dakika ya 36 na Mshambuliaji Waziri Junior Shentembo.

    Hii ni mara ya tatu kwa Toto Africans kuitambia Mwadui FC katika michezo ya ufunguzi wa pazia la ligi kuu bara.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: LIGI KUU BARA:TOTO AFRICANS YAIZIMA MWADUI FC CCM KIRUMBA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top