728x90 AdSpace

Friday, August 26, 2016

BAADA YA KUNYIMWA KIBALI,TAKUMA WA ARSENAL ATIMKIA UJERUMANI


Stuttgart,Ujerumani.

BAADA ya kushindwa kupata kibali cha kucheza soka Uingereza,Arsenal,imemtoa kwa mkopo wa msimu mmoja Mshambuliaji wake Mjapan Takuma Asano kwenda VFB Stuttgart inayoshiriki ligi daraja la pili nchini Ujerumani.

Takuma,21,alijiunga na Arsenal mwezi Julai kwa dau la £5m akitokea Sanfrecce Hiroshima ya nyumbani kwao Japan lakini kutokana na kushindwa kukidhi vigezo vya kucheza soka nchini Uingereza amelazimika kujiunga na VFB Stuttgart kwa mkopo wa msimu mmoja ili kupata uzoefu wa kucheza soka Ulaya pamoja na kujiongezea sifa za kucheza ligi kuu nchini Uingereza.


  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: BAADA YA KUNYIMWA KIBALI,TAKUMA WA ARSENAL ATIMKIA UJERUMANI Rating: 5 Reviewed By: Unknown