728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, August 31, 2016

    RASMI:DAVID LUIZ AREJEA CHELSEA


    London,Uingereza.

    HATIMAYE Chelsea imemsajili kwa mara ya pili beki wa kimataifa wa Brazil,David Luiz,lakini safari hii akitokea Paris Saint-Germain ya Ufaransa kwa ada ya £38m (€45m).

    Luiz mwenye umri wa miaka 29 sasa amerejea Chelsea ikiwa ni miaka miwili tu imepita tangu aihame klabu hiyo na kujiunga na Paris Saint-Germain kwa ada ya £50m.

    Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa juu ya urefu wa mkataba aliosaini beki huyo mwenye uwezo wa kucheza pia kama kiungo wa ulinzi.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RASMI:DAVID LUIZ AREJEA CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top