728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, August 26, 2016

    MPANGO WA PLUIJM LIGI KUU BARA HUU HAPA


    KOCHA wa Yanga, Hans van Pluijm amesema atatumia Ligi Kuu Bara kama maandalizi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani.

    Akizungumza jana Pluijm alisema kilichowaangusha kwenye michuano ya msimu huu ni wachezaji wake kukosa uzoefu lakini kwa sasa wameshaiva hivyo mwakani anatarajia kufanya vizuri zaidi.

    “Mwakani sitaki tena kushuka na kucheza shirikisho, lengo langu ni kuhakikisha tunafanya vizuri klabu bingwa na kucheza hatua ya nane bora na si vinginevyo, kilichotufanya tukashuka shirikisho ni wachezaji wangu kukosa uzoefu,” alisema Pluijm.

    “Tulikosa uzoefu, tukajikuta tunafungwa hata nyumbani, ilipaswa kupata ushindi kwenye mechi za nyumbani, pia tulifanya makosa mengi kwenye safu yetu ya ulinzi na hiyo ndiyo ilitufanya tufungwe mabao ambayo mengine ni ya kizembe… “Kiukweli mechi za nyumbani ni lazima ushinde, usipofanya hivyo kwako unadhani utawezaje ugenini, tayari nimeshaongea na wachezaji wangu kusahau yaliyopita, tujipange kwa kutetea ubingwa na hapo hapo tutumie ligi kujinoa zaidi kwa ajili ya klabu bingwa mwakani,” alisisitiza.

    “Nitatumia michuano ya Ligi kama moja ya maandalizi ya michuano ya klabu bingwa mwakani na pia kuhakikisha tunatetea ubingwa wetu,” alisema.

    Yanga itaanza harakati zake za kutetea ubingwa huo katika mchezo dhidi ya African Lyon kesho kutwa katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

    Katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Yanga ilifungashiwa virago na Al Ahly ya Misri baada ya kuchezea kichapo cha mabao 2-1 wakiwa ugenini na kuangukia kucheza Kombe la Shirikisho ambalo nalo wameshatupiwa virago.

    Kabla ya mchezo wao wa mwisho dhidi ya TP Mazembe ambayo walikula kichapo cha mabao 3-1 mapema wiki hii, Yanga ilikuwa tayari imeshacheza mechi tano dhidi ya MO Bejaia, Medeama na TP Mazembe na kufungwa tatu, sare moja na kushinda moja, ikikusanya pointi nne.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MPANGO WA PLUIJM LIGI KUU BARA HUU HAPA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top