728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, August 24, 2016

    WENGER KUMUUZA SANCHEZ KWENDA REAL MADRID KWA MASHARTI MAWILI

    London,Uingereza.

    KOCHA wa Arsenal,Arsene Wenger,ameonyesha nia ya kutaka kuwauzia Real Madrid nyota wake raia wa Chile,Alexis Sanchez,katika kipindi hiki cha usajili ama kile cha mwezi Januari lakini kwa sharti la yeye kupewa wachezaji wawili.

    Kwa mujibu wa gazeti la Don Balon ni kwamba wachezaji wanaotakiwa na kocha Arsene Wenger ni Mcolombia James Rodriguez pamoja na Mhispania Alvaro Morata.

                                                                                  Alvaro Morata

    Don Balon limeendelea kupasha kuwa Arsenal imesema kuwa katika dili lolote lile la kumtaka Sanchez lazima Real Madrid imjumuishe mshambuliaji wake Alvaro Morata,vinginevyo hakutafanyika biashara ya aina yoyote ile.

    Wakati huohuo taarifa kutoka nchini Italia zinasema Inter Milan nayo imejitosa kumwania Sanchez na tayari imeshaandaa ofa ya €80m ili kuhakikisha inamsajili katika kipindi hiki cha usajili barani Ulaya.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WENGER KUMUUZA SANCHEZ KWENDA REAL MADRID KWA MASHARTI MAWILI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top