CAIRO,MISRI.
SHIRIKISHO la soka Barani Afrika (CAF) limemzuia beki mpya wa Yanga SC, Hasann Kessy kucheza mchezo wa kesho Jumapili wa kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Mo Bejaia utakaochezwa huko Bejaia,Algeria mishale ya saa 6:15 Usiku.
Taarifa kutoka Misri yaliko makao makuu ya shirikisho hilo zinasema CAF itamruhusu Kessy kucheza michuano ya shirikisho mpaka hapo klabu yake ya zamani ya Simba SC itakapotoa barua kuthibitisha kuwa beki huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar alimaliza mkataba wake na imeridhia achezee Yanga SC.
0 comments:
Post a Comment