Naandika barua hii kuishukuru familia nzima ya Manchester United kwa kuniunga mkono kwa mwaka mmoja niliokuwa sehemu ya klabu.
Manchester
United waliponichagua kuwa sehemu ya timu yao, nilijisikia kuheshimiwa
kwasababu nilijua klabu hii ina maanisha nini na jinsi gani iliniamini.
Hata hivyo, nafahamu mambo hayakwenda vizuri kama tulivyotarajia, naomba msamaha kwa hilo.
Katika maisha ya mcheza mpira, kuna wakati mwingine mambo usiyotarajia na usiyoyataka yanatokea.
Nawahakikishia
kwamba haikuwa kujaribu. Nilijitahidi niwezavyo, lakini mpira sio kama
hesabu: Mara zote kuna vitu vingi vinavyoathiri vile unavyofikiria.
Samahani sana kwasababu sikufanya kile nilichotarajia katika klabu hii kubwa na ya ajabu.
Natoa
shukurani za pekee kwa bodi ya wakurugenzi na utawala ya Manchester
United, vilevile kila kiongozi na wachezaji wenzangu walioniunga mkono.
Pia shukurani za pekee ziwaendee mashabiki ambao mara zote waliniamini na kuonesha heshima na mapenzi makubwa.
Sasa ni wakati wa kujiunga na PSG, lakini Utukufu wa Manchester United utabaki kwenye kumbukumbu zangu daima.
Nawatakia kila la kheri
0 comments:
Post a Comment