Mshambuliaji wa Vital’O ya Burundi, Laudit Mavugo, sasa amethibitisha kwa 100% kufa kw dili lake na Simba baada ya kurejesha fedha za awali alizopewa na Wekundu hao.
Mavugo ambaye awali alionyesha kutoafiki suala la kurejesha fedha hizo akiamini lolote linaweza kutokea, amebadili mawazo na kurudisha ‘advance’ dola 10,000 (Sh milioni 20) aliyotanguliziwa na Simba kwa makubaliano ya kumaliziwa dola 10,000 nyingine baada ya kusaini.
Dili la Mavugo na Simba liliku baada ya Vital’O kuongeza dau usajili la mchezaji huyo kutok Sh milioni 120 mpaka 200 baada ya kuelezwa kuwa timu kibao zinamtolea udenda, hiyo ikaifa Simba kukaa kando na kuangalia mipango mingine.
Mtu wa ndani wa Simba amesema ishu hiyo na jinsi walivyoahidiana na Mavugo kama itatokea wakati mwingine wakihitaji huduma yake.
“Ameturejeshea ile pesa tuliyo bila ya tatizo na tumemalizana naye, tumeelewana kuwa kama baadaye tunaweza kuhitaji hudu yake basi tutakamilisha hilo k wepesi zaidi maana hata hatukuelewa kilichotokea kwa Vital’O kwenye dakika za mwisho,” alisema bosi huyo.
0 comments:
Post a Comment