728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, August 14, 2016

    WENYEJI BRAZIL NAO WATINGA NUSU FAINALI OLIMPIKI


    Corinthians, Brazil.

    BRAZIL U23 imefanikiwa kufuzu nusu fainali ya michuano ya Olimpiki kwa upande wa soka la wanaume baada ya leo alfajiri kuifunga Colombia U23 kwa jumla ya mabao 2-0 katika mchezo wa robo fainali uliochezwa katika uwanja wa Arena Corinthians.

    Brazil imepata mabao yake kupitia kwa nahodha wake,Neymar 14' aliyefunga kwa mkwaju wa faulo pamoja na Luan 85'

    Brazil sasa itacheza na Honduras katika mchezo wa nusu fainali utakaochezwa siku ya Jumatano.Honduras imefika hatua hiyo baada ya kuichapa Korea Kusini kwa bao 1-0 lililofungwa na A Elis dakika ya 58 huko Estadio Mineirao.

    Vikosi

    Colombia: Bonilla, Tesillo, D.Balanta,Lerma, Pabon,Gutierrez (C), Preciado,Roa, Palacios, Barrios, C.Borja

    Brasil: Weverton, Zeca, R.Caio,Marquinhos, R.Augusto, D.Santos, Luan,G.Barbosa, Neymar (C), G.Jesus,Walace

    Timu zilizotinga nusu fainali ni Ujerumani,Brazil,Nigeria na Honduras

    Ratiba ya Nusu fainali Jumatano

    Ujerumani v Nigeria

    Brazil v Honduras




    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WENYEJI BRAZIL NAO WATINGA NUSU FAINALI OLIMPIKI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top