728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, July 19, 2016

    LIGI KUU BARA KUANZA AGOSTI 20,YANGA SC YAANZA NA KIPORO

    Dar es Salaam,Tanzania.

    Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa msimu wa 2016/17 inatarajiwa kuanza kutimua vumbi lake kuanzia Agosti 20 mwaka huu ambapo Agosti 17 itatanguliwa na mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya Yanga SC na Azam FC

    Kwa ujumla Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2016/ 2017
    itaanza Agosti 20,Simba SC wakifungua dimba na Ndanda FC Uwanja wa
    Taifa, Dar es Salaam, huku Azam wakiikaribisha African Lyon Uwanja wa
    Azam Complex, Chamazi,
    Dar es Salaam.

    Mechi nyingine za ufunguzi zitakuwa kati ya Kagera Sugar na Mbeya City
    Uwanja wa Kaitaba,Bukoba, Toto Africans na Mwadui FC Uwanja wa
    CCM Kirumba, Mwanza,Stand United na Mbao FC Uwanja wa Kambarage,
    Shinyanga, Mtibwa Sugar na Ruvu Shooting Uwanja wa Manungu, Turiani,
    Morogoro na Majimaji na Prisons Uwanja wa Majimaji Songea.

    Mabingwa wa Ligi hiyo,Yanga watafungua dimba na JKT Ruvu Agosti 31 badala ya Agosti 20/21 Uwanja wa Taifa kutokana na kukabiliwa na pambano la ugenini dhidi ya TP Mazembe Agosti 23.

    RATIBA KAMILI IKO KAMA IFUATAVYO

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: LIGI KUU BARA KUANZA AGOSTI 20,YANGA SC YAANZA NA KIPORO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top