728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, July 28, 2016

    GUARDIOLA NA MAN CITY YAKE WAICHAPA DORTMUND 6-5 ICC

    Shenzhen,China.

    KOCHA Pep Guardiola ameiongoza klabu yake mpya ya Manchester City kuichapa Borussia Dortmund kwa penati 6-5 katika mchezo mkali wa kimataifa wa kirafiki wa michuano ya International Champions Cup (ICC) ulioisha hivi punde katika uwanja wa Shenzhen Longgang,China.

    Mchezo huo ulilazimika kuamuliwa kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada timu hizo kwenda sare ya kufungana bao 1-1 katika muda wa kawaida.

    Sergio Aguero alianza kuifungia Manchester City bao la kuongoza dakika ya 79 kabla ya Christian Pulisic kuifunga Borussia Dortmund bao la kusawazisha dakika ya 96 na kupelekea mshindi atafutwe kwa changamoto ya mikwaju ya penati na ndipo Manchester City walipoibuka wababe kwa penati 6-5 baada mlinda mlango wake Angus Gunn kupangua penati ya Mikel Merino wa Borussia Dortmund.

    VIKOSI

    Man City: Caballero (Gunn) |
    Adarabioyo, Otamendi (Maffeo),Kolarov (Angelino) | Navas (Silva),Fernandinho,Fernando (Toure (Sterling)), Clichy (Denayer) | Zinchenko (Aleix García), Delph (Agüero) | Iheanacho (Bony (Nolito))

    Borussia Dortmund : Bürki | Ginter (Merino), Bartra (Larsen), Sokratis (Bender), Schmelzer (Passlack) | Rode (Castro), Sahin (Bumic) | Mor (Pulisic), Leitner, Dembele (Kagawa) |Ramos (Hober)

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: GUARDIOLA NA MAN CITY YAKE WAICHAPA DORTMUND 6-5 ICC Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top