728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, July 22, 2016

    MAN UNITED YAANZA VIBAYA MICHUANO YA ICC YACHAPWA 4-1 NA DORTMUND

    Shanghai, China.

    MANCHESTER United imeianza vibaya Michuano ya International Champions Cup (ICC) baada ya jioni ya leo kukubali kichapo cha mabao 4-1 toka kwa Borussia Dortmund katika mchezo Mkali uliochezwa katika Uwanja wa Shanghai ulioko Shanghai, China.

    Mabao yaliyoipa Ushindi Borussia Dortmund katika mchezo wa leo yametiwa kimiani na Gonzalo Castro aliyefunga mara mbili dakika za (19) na (85),Pierre-Emerick Aubameyang dakika ya (36) kwa mkwaju wa penati na kinda Ousmane Dembele dakika ya (57).

    Bao la kufutia machozi la Manchester United limefungwa dakika ya (59) na Henrik Mkhitaryan​ baada ya kupokea pasi murua kutoka kwa Juan Mata.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAN UNITED YAANZA VIBAYA MICHUANO YA ICC YACHAPWA 4-1 NA DORTMUND Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top