728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, July 26, 2016

    PIGO:BEKI ARSENAL NJE MIEZI MITANO

    London, England.

    BEKI wa Arsenal,Per Mertesacker,anatarajiwa kukaa nje ya dimba kwa kipindi cha miezi mitano baada ya kupata jeraha la goti



    Mertesacker,31,alipata jeraha hilo Ijumaa iliyopita wakati akiichezea Arsenal katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya RC Lens ya Ufaransa ulioisha kwa sare ya bao 1-1.

    Kuumia kwa Mertesacker ni pigo kwa kocha wa Arsenal Mfaransa,Arsene Wenger,ambaye hivi karibuni alitarajia kumtangaza beki huyo wa zamani wa Weder Bremen kuwa nahodha mpya wa klabu hiyo kufuatia kuondoka kwa Mhispania,Mikel Arteta aliyejiunga na benchi la ufundi la Manchester City.

    Wakati huohuo,Mertesacker,ameachwa katika kikosi cha Arsenal kilichosafiri Jana mchana kwenda Marekani kucheza michezo ya kimataifa ya kujipima nguvu.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PIGO:BEKI ARSENAL NJE MIEZI MITANO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top