728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, July 30, 2016

    NDOA TBL,SIMBA YAFIKIA MWISHO

    Dar es Salaam,Tanzania.

    KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) imeamua kutosaini mkataba wa kuendelea kuidhamini Simba.
    Taarifa kutoka ndani ya Simba, zinaeleza TBL imegoma kusaini mkataba ikionekana kuingia hofu baada ya Yanga kutotaka kuendelea nao au waingie wakiwa na ofa mpya.

    Pamoja na hiyo imeelezwa kumekuwa na juhudi binafsi zinazofanywa na baadhi ya viongozi kujaribu kuwashawishi TBL kupitia Kilimanjaro, wabadili uamuzi.

    Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Simba, Patrick Kahemele alisema jana mkataba huo na TBL unamalizika mwishoni mwa mwezi ujao na Simba haina mpango wa kuongeza tena.

    Kahemele alisema kuwa makampuni kibao makubwa hapa nchini yanagombea kuingia mkataba na Simba na klabu hiyo inatafakari nani wa kuingia naye mkataba kutokana na fungu kubwa la fedha.

    Alisema Simba ni timu kubwa na makampuni mengi yanataka kuingia nayo mkataba, hivyo ule wa TBL ulikuwa mdogo na unamalizika mwishoni mwa mwezi ujao.

    Alisema baada ya kumalizika kwa mkataba huo, Simba itatangaza makampuni yanayotaka kufanya biashara na Simba.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: NDOA TBL,SIMBA YAFIKIA MWISHO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top