728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, July 25, 2016

    WAMEPONA:MPAMBANO WA MAN UNITED NA MAN CITY ULIOKUWA UPIGWE LEO MCHANA NCHINI CHINA UMEFUTWA

    Beijing, China.

    ILE hamu ya mashabiki wa vilabu vya Manchester United na Manchester City kuona vilabu vyao vikipepetana leo mchana katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki wa michuano ya ICC imeingia nyongo baada ya pambano hilo kufutwa kutokana na hali mbaya ya hewa kulikumba jiji la Beijing ambalo lilipangwa kuwa mwenyeji wa mpambano huo.

    Taarifa kutoka Beijing,China zinasema uamuzi huo umefikiwa baada ya waandaaji wa michuano hiyo pamoja na wakuu wa vilabu hivyo viwili kufikia makubaliano kuwa mchezo huo ufutwe baada ya mvua zinazoendelea kunyesha jijini humo kuharibu miundombinu ya uwanja hali ambayo inatishia afya za machezaji ikiwemo kupata majeraha.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WAMEPONA:MPAMBANO WA MAN UNITED NA MAN CITY ULIOKUWA UPIGWE LEO MCHANA NCHINI CHINA UMEFUTWA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top