728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, July 23, 2016

    MBEYA CITY YACHOMOA MMOJA KUTOKA COASTAL UNION

    Mbeya,Tanzania.

    KLABU ya MBEYA City yenye Makao yake Makuu jijini Mbeya imetangaza kumsajili kwa Mkataba wa Miaka miwili Kiungo Fundi, Ayoub Idrisa Semtawa kutoka Klabu ya Coastal Union ya jijini Tanga. 

    Mbeya City imeamua kumsajili Ayoub Idrisa Semtawa baada ya kukoshwa na kiwango kizuri alichokionyesha msimu uliopita katika michezo ya ligi kuu bara na ile ya shirikisho maarufu kama kombe la Azam FA Cup.


    Ayoub anakuwa mchezaji
    wa pili kujiunga na Mbeya
    City katika kipindi kisichozidi wiki moja,hii ni baada ya mapema wiki hii
    Mbeya City kumsajiliwa beki wa Yanga,Rajab Zahir aliyekuwa anacheza kwa mkopo Stand United.fbbm
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MBEYA CITY YACHOMOA MMOJA KUTOKA COASTAL UNION Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top