728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, June 15, 2016

    COPA AMERICA CENTENARIO:ARGENTINA,CHILE ZAVUNA USHINDI MKUBWA NA KUFUZU ROBO FAINALI,SASA KUVAANA NA WAPINZANI HAWA

    Washington,Marekani.

    ARGENTINA na Chile zimefanikiwa kuwa timu pekee kutoka kundi D kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya Copa America Centenario baada ya Alfajiri ya leo kupata ushindi mkubwa dhidi ya Bolivia na Panama.

    Argentina wakiwa katika dimba la CenturyLink Field, Seattle,huko Washington wameifunga Bolivia kwa mabao 3-0.Mabao hayo yametiwa kimiani na Erik Lamela 13',Ezequel Lavezzi 15' na msumali wa mwisho ukipigwa na Victor Cuesta 32'

    Katika mchezo mwingine wa kundi D,Chile imeifunga Panama kwa mabao 4-2.Mabao ya Chile yamefungwa na Eduardo Vargas na Alexis Sanchez wote wamefunga mara mbili.Panama wao wamepata mabao yao kupitia kwa Miguel Camargo na Abdiel Arroyo

    Ratiba ya robo fainali 

    Argentina vs Venezuela

     Chile v Mexico 


    Marekani v Ecuador

    Peru v Colombia
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: COPA AMERICA CENTENARIO:ARGENTINA,CHILE ZAVUNA USHINDI MKUBWA NA KUFUZU ROBO FAINALI,SASA KUVAANA NA WAPINZANI HAWA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top