Hizi ni taarifa mbaya kwa mashabiki wa Arsenal wakati huu timu yao inaelekea kuanza msimu mpya wa ligi kuu England ikiwa na matumaini ya kuipindua Chelsea.
Arsenal chini ya Arsene Wenger
wanaamini sasa umefika wakati wa kuchukua ubingwa ambao upo mikononi mwa Jose
Mourinho.Hata hivyo, hofu imetanda Emirates
baada ya vipimo kuonesha kwamba Jack Wilshere anaweza kukaa nje ya uwanja
wa muda mrefu baada ya kuonekana kuna jeraha kubwa katika kifundo chake cha
mguu alichoumia.
Arsenal wanatarajia kufanya zaidi
mwishoni mwa juma hili, lakini hali inavyoonesha Wilshere anaweza kukaa nje ya
uwanja kwa wiki sita hadi nane.
0 comments:
Post a Comment