728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, February 22, 2017

    Liverpool na Real Madrid Vitani Kumwania Brandt

    Na Faridi Miraji.                                            

    Liverpool wanajiandaa kula sahani moja na Real Madrid kwenye mbio za kuwania saini ya winga wa kimataifa wa Ujerumani Julian Brandt.

    Klabu hiyo ya jiji la Merseyside wameripotiwa kutuma Maskauti kwenda kumuangalia Brandt,20 akiwa na kikosi chake cha Bayer Leverkusen kwenye mechi ya UEFA dhidi ya Atletico Madrid jana usiku 

    Maendeleo ya ukuaji wa kasi wa kiwango cha soka cha  Brandt yamevutia vilabu vingi vikubwa barani Ulaya ikiwemo Real Madrid, lakini Klopp ana matumaini ya kumpeleka winga huyo Anfield.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Liverpool na Real Madrid Vitani Kumwania Brandt Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top