728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, February 27, 2017

    Simba SC yatoa tano kwa mashabiki wake na serikali

     
     James Eduma.
     
    Dar Es Salaam,Tanzania.
     
    Uongozi wa klabu ya Simba umetoa shukurani kwa mashabiki na wanachama wao kwa ustaarabu waliouonyesha wakati wa mchezo wao dhidi ya Young Africans ambao ulimalizika kwa kupata ushindi wa mabao mawili kwa moja.
     
    Shukurani kwa mashabiki na wanachama wa Simba zimetolewa na mkuu wa idara ya habari na mawasiliono Haji Manara alipozungumza na vyombo vya habari mchana wa leo kwenye ukumbi wa kamao makuu ya klabu hiyo yaliopo Mtaa wa Msimbazi Dar es salaam.
     
    Haji amesema mashabiki na wanachama wa Simba walionyesha ustaarabu wa hali ya juu kutokana na maamuzi yaliyochukuliwa dhidi ya kikosi chao ambayo yalikua halali tangu dakika ya kwanza hadi mwisho.

    Hata hivyo Haji Manara ametoa wito kwa mashabiki na wanachama wa Simba kuendelea kuwa kitu kimoa katika kipindi hiki cha kuelekea mwishoni mwa msimu huu, na pia amewataka kufika viwanjani bila kusita kuishangilia timu yao ili iweze kuhitimisha azma ya kutwaa ubingwa kwa kushinda michezo saba ya ligi iliyobaki.

    Wakati huo huo Manara ametoa shukurani kwa Serikali, taasisi na watu mbali mbali ambao walihakikisha mchezo wa jumamosi unachezwa kwa amani na utulivu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Simba SC yatoa tano kwa mashabiki wake na serikali Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top