728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, February 27, 2017

    Sunday Manara "Computer" awapa vidonge vyao wachezaji Yanga SC

    Dar Es Salaam,Tanzania.

    Aliyekua mshambuliaji wa klabu ya Young Africans pamoja na timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Sunday Manara amewatuhumu wachezaji wa klabu hiyo kwa kusema hawakutambua umuhimu wa mchezo wao wa jumamosi dhidi ya Simba na badala yake wakashindwa kutumia muda na nafasi walizozipata.

    Sunday Manara ambaye ni baba mzazi wa afisa habari wa Simba Haji Manara amesema Yanga walipaswa kuwa na nidhamu ya mchezo wakati wote kwa kucheza soka bila kuwadharau wapinzani wao, lakini walishindwa kutimiza wajibu huo wakajikuta wakiadhibiwa na kupoteza point tatu.

    Akitolea mfano kwa upande wa Simba, mwanasoka huyo wa zamani amesema kilichowasaidia Simba ni kutovunjika moro na kutumia ari waliyokua nayo, jambo mbalo lilikosekana kwa Young Africans ambao walionyesha kucheza kwa mazoea.



    Hata hivyo Sunday manara ambaye alibahatika kuwa mtanzani wa kwanza kucheza soka la kulipwa barani Ulaya, amewakumbusha baadhi ya mashabiki na wanachama wa Young Africans ambao wameanza kumnyooshea kidole kocha George Lwandamina kwa kusema hafai, kwa kusema wakumbuke mfumo unaotumiwa na viongozi wao kwa sasa.

    Sunday amesema mfumo na mikakati ya kuwa na wachezaji tangu wakiwa na umri mdogo ambao wanaweza kukuzwa ndani ya klabu hiyo umeachwa hivyo kinachofanyika kwa sasa ni kuwategemea wachezaji wakigeni ambao wanaonekana kuchoka kutokana na kutumikiswa kila siku.



    Kuhusu harufu ya ubingwa ambayo inaelekezwa Msimbazi baada ya matokeo ya mabao mawili kwa moja siku ya jumamosi, Sunday manara amesema bado ni mapema mno kufikiria suala hilo, japo amekiri tofauti ya point tano iliopo sasa kati ya Simba na Yanga inaweza ikawa chanzo kwa Wekundu wa Msimbazi kujifuta machozi ya kukosa taji la Tanzania bara kwa miaka mitano iliyopita.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Sunday Manara "Computer" awapa vidonge vyao wachezaji Yanga SC Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top