728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, February 26, 2017

    Sevilla yaishusha Barca,yaikamata Real Madrid kileleni La Liga


    Sevilla,Hispania.

    SEVILLA wametoka nyuma na kuwachapa watani wao wa jadi Real Betis mabao 2-1 kwenye mchezo mkali wa La Liga wa 'El Gran Derbi' uliochezwa kwenye dimba la Estadio Benito Villamarin ,Jumamosi usiku.

    Wenyeji Real Betis ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza baada ya mlinzi wake wa kushoto, Riza Durmisi kufungwa kwa mkwaju wa faulo katika dakika ya 36 ya mchezo.

    Lakini mabadiliko yaliyofanywa kipindi cha pili na kocha wa Sevilla, George Sampaoli ya kuwaingiza nahodha Vicente Iborra na Wissam Ben Yedder yaliipa matumaini miamba hiyo ambapo ilifanikiwa kupata mabao mawili yaliyofungwa na Gabriel Mercado katika dakika ya 56 na Vicente Iborra kwa kichwa katika dakika ya 76 ya mchezo.

    Ushindi huo umeifanya Sevilla ichupe mpaka nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ya La Liga ikiwa na pointi 52 sawa na vinara Real Madrid wenye michezo miwili mikononi.Mabingwa watetezi Barcelona wako nafasi ya tatu wakiwa na pointi 51.

    Michezo ya leo La Liga

    Atletico Madrid v Barcelona 12:00 jioni
    Virrareal v Real Madrid


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Sevilla yaishusha Barca,yaikamata Real Madrid kileleni La Liga Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top