728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, February 18, 2017

    Zanaco yaitupa nje APR, sasa kuivaa Yanga SC klabu bingwa Afrika

    Kigali,Rwanda.

    BAO la dakika ya 17 la mlinzi wa Zanaco,Taonga Bwembya limetosha kuitupa APR nje ya michuano ya klabu bingwa Afrika baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0 katika mchezo mkali wa mkondo wa pili uliochezwa jioni ya leo huko Amahoro,Kigali. 

    Ikumbukwe katika mchezo wa awali uliochezwa huko Lusaka,Zambia timu hizo zilishindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya 0-0.

    Sasa hii ina maana kwamba Zanaco itacheza na mabingwa wa Tanzania,Yanga SC kwenye hatua inayofuata hapo Machi 11.Yanga SC imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa mabao 6-2 dhidi ya Ngaya FC ya Comoro.Mshindi kati ya Yanga SC na Zanaco atatinga hatua ya makundi.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Zanaco yaitupa nje APR, sasa kuivaa Yanga SC klabu bingwa Afrika Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top