728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, February 27, 2017

    Yanga SC yaomba radhi kufuatia kipigo cha 2-1 kutoka kwa Simba SC

     
     
    James Eduma.

     Dar Es Salaam,Tanzania.

    Wanachama na mashabiki wa Young Africans wameombwa radhi kufuatia kupoteza mchezo wa wao wa siku ya jumamosi kwa kukubali kufungwa na watani zao Simba kwenye mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania bara.
     
    Katibu mkuu wa Young Africans amewasilisha kauli ya kuomba radhi kwa mashabiki na wanachama kwa niaba ya uongozi wa juu wa klabu hiyo ambayo bado inaendelea kutetea ubingwa wa Tanzania bara.
     
    Mkwasa amesema imeulazimu uongozi wa Young Africans kufanya hivyo kutokana na kuamini kila mmoja alisikitishwa na matokeo ya mchezo huo, ambao ulishuhudia wakiongoza bao moja kwa kipindi kirefu.

    Hata hivyo mkwasa amesema kufungwa katika mchezo wa jumamosi dhidi ya Simba hakujawaondoa kwenye malengo ya kuendeleza mazuri katika michezo mingine ya ligi kuu, hivyo amewataka wanachama na mashabiki kuendelea kuwa wastahamilivu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Yanga SC yaomba radhi kufuatia kipigo cha 2-1 kutoka kwa Simba SC Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top